Sunday, May 10, 2009

Mkenya daima

Wakati umefika pale ambapo wakenya wanafaa kuelewa kila kitu kuhusu uendeshaji serikali na haki zao. Wakenya wafaa kuhusishwa moja kwa moja kwa sababu sio wanasiasa ndio wanaofaa kuwaamulia.

Hebu tafakari, wanasiasa walisema wamatuwakilisha; Je, wanapopata rushwa, wanatuwakilisha? Wanapolala bungeni je?

Si dhani kuna nia ya kuchagua yeyote asiyeshughulikia matakwa ya raia.

Mkenya daima.

Monday, April 27, 2009

Siku ya wafanyikazi


Siku ya wafanyikazi ulimwenguni imewadia. Tarehe mosi mwezi wa tano viongozi watapiga kelele kama ilivyokuwa jadi.

Wafanyikazi bado wanabaguliwa kwa kupewa marupurupu tofauti, au kuwa na mishahara midogo huku wengine wakinyanyaswa hata kijinsia. Mazingira ya kazi bado ni duni.

Je, vio
ngozi, au serikali wametimiza walioahidi mwaka jana?

* Picha imepigwa na Natall news

Friday, April 10, 2009

Is Easter, or other religious holidays turning secular?

Easter holiday is filling our esophagus with much fun, and remembrance of the betrayal, death and resurrection of Jesus Christ. For the Catholics, it will be another time for pilgrim; the Pentecostals will be discharging heavy music bangs to the atmosphere, and have something to dance to. The Muslims will just have more days to rest, while the atheists will have extra time to engage Christians questioning the existence of God.

Whatever category you fall in, have religious holidays become more dotted with sin, or more secular?

Monday, December 08, 2008

NIPE KITABU kwenye BBC Kiswahili

Jana jioni nilisogea redio yangu ili kusikiliza kipindi cha NIPE KITABU kwenye BBC-Kiswahili.

Mwendesha kipindi Aisha Yahya na Profesa kutoka Chuo cha Dar es salaam waliangazia kazi za Shaban Robert, mwandishi anayesifika sana ulimwenguni, hasa katika uchapishaji kwa lugha ya Kiswahili.

Kuzidi hayo, Profesa aliguzia jitihada za chuo cha Dar kuchapisha kazi zingine asili za Shaban bila kuhaririwa hivi karibuni. Kazi hizo zikichapishwa usikokose kununua mpenda Kiswahili.

Kwangu mimi, NIPE KITABU ni kipindi kizuri sana, na itakuwa vyema kama tungeelezewa mapema wageni wa kipindi hicho moja kwa moja, au wakiundie blogu.

Usikose wiki ijayo...

Wednesday, June 25, 2008

Suluhu ya njaa barani ni ipi?

Siku zinayoyoma huku nambari ya watu wanaoaga kutokana na njaa katika pembe ya Afrika yaongezeka. Somalia imehadhirika zaidi kutokana na upungufu wa mvua na machafuko ya kivita inayozuia ugawanyaji wa chakula.

Takwimu za umoja wa mataifa (UN) zaonyesha watu milioni 14.5 million wanahitaji msaada wa kibinadamu kwa haraka. Idhaa ya BBC inaripoti kuwa watoto wengi wanautapiamlo.

Ripoti hizi zinauzito mwingi sana, lakini mbona ulimwengu haukimbii kuinisuru Somalia? Jibu kwa swala la upungufu wa chakula barani ni nini ilhali Afrika ni kikapu cha chakula ulimwenguni?

Friday, April 18, 2008

Kony atatia saini iwapo...

Sakata ya kiongozi wa Lord Resitance Army (LRA), Joseph Kony kutosaini mkataba wa amani inaonekana kuwa shtuo kwa wanauganda, raia na viongozi wa pembe ya Afrika.

Kony anataka kufafanuliwa vipengee kadhaa katika mkataba, na amewaomba viongozi wa kitamaduni na wa dini kumsaidia.

Wiki jana, David Matsanga mjumbe mkuu katika mazungumzo ya amani kati LRA na serikali ya Uganda huko Juba, Sudan Kusini alijiuzulu. Matsanga alidai hana umuhimu kwa sasa kwani alishindwa kumbembeleza Kony kusiaini mkataba.

Wiki hii Kony alimwapisha Jame Obita kama kiongozi wa wajumbe wake katika mazungumzo ya amani. Jambo ambalo lilikaribishwa mno na serikali ya Uganda.

Je, nini kinamzuia Kony kusaini mkataba?

Kony anahofia kufikishwa katika mahakama ya kimataifa ya jinayi (ICC). Kwa sasa hana uhakikisho kwamba atahukumiwa katika makama za Uganda. Akirusha mawazo yake, anamwona Charles Taylor wa Liberia kizimbani huko Hague. Akilala, anamwona Slobodan Milosevic wa Kosovo kizimbani.

Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni kusema Kony awezi kufikishwa Hague haipendezi, kwani waranta ya Kony kushikwa na kufikishwa ICC ipo.

Kwa muda sasa, ni wazi kwamba Kony hamwamini yeyote yule. Tunakumbuka vifo alivyovisababisha kwa manaibu waki, kama vile, Vincent Otti na Okot Odhiambo.

Kwa kifupi, Kony ataweza kusaini mkataba wa amani utaomaliza vita vilivyodumu kuzidi miaka ishirini, iwapo atahakikishwa hatafikishwa Hague.

Tuesday, January 08, 2008

Sauti