Monday, December 08, 2008

NIPE KITABU kwenye BBC Kiswahili

Jana jioni nilisogea redio yangu ili kusikiliza kipindi cha NIPE KITABU kwenye BBC-Kiswahili.

Mwendesha kipindi Aisha Yahya na Profesa kutoka Chuo cha Dar es salaam waliangazia kazi za Shaban Robert, mwandishi anayesifika sana ulimwenguni, hasa katika uchapishaji kwa lugha ya Kiswahili.

Kuzidi hayo, Profesa aliguzia jitihada za chuo cha Dar kuchapisha kazi zingine asili za Shaban bila kuhaririwa hivi karibuni. Kazi hizo zikichapishwa usikokose kununua mpenda Kiswahili.

Kwangu mimi, NIPE KITABU ni kipindi kizuri sana, na itakuwa vyema kama tungeelezewa mapema wageni wa kipindi hicho moja kwa moja, au wakiundie blogu.

Usikose wiki ijayo...

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home