Sunday, November 25, 2007

Uganda: Aibu yaikumba upinzani

Wiki jana Kampala, Uganda, ilijaa na wageni kutoka nchi 52 zilizoko katika jumuiya ya nchi za madola.


Malkia Elizabeth wa pili wa Uingereza alikuwa mgeni wa heshima katika mkutano huo.

Cha kustajaabisha ni vile vyama vya upinzani badala na kufanya wageni wahisi nyumbani waliamua kufanya migomo. Serikali ya Uganda iliwapa ruhusa kufanya mgomo katika kiwanja cha ndege cha Kololo lakini vyama vilipuuza na kuamua kuingia jijini.

Polisi wa kizima ghasia hawakusita kuwacharaza waliovunja sheria.

Kulingana na mimi, badala ya kufanya migomo viongozi wa upinzani wakijiandaa kupatana na Malkia na wageni kutoka mataifa mengine, aghalabu waelezee matatizo ya kwa njia ya kistaarabu.

Pole sana upinzani kwa kukosa mwelekeo na sijui kama mtapata nafasi ya kunena na wageni tena.

Ukidhani ni vyama vya upinzani tu vilivyogoma utakuwa umekosea. Wafalme wa Buganda na Bunyoro walidinda kupatana na Malkia Elizabeth wakidai kwamba ni lazima wasuluhishe madhambi ambayo Uiengereza ilifanyia falme hizi.

Swali kwa falme hizo, Malkia Elizabeth alikuwa wa wadhifa alio nao wakati madhambi yalikuwa yakifanyika? Je, falme zingepeleka kesi zao kati mahakama ya kimataifa, siwangepata suluhu?

Picha/timesonline.co.uk

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home